Tanzania
Sheria ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2022
Tenda 6 ya 2022
- Imechapishwa katika Government Gazette 39 hadi 7 Oktoba 2022
- Imeidhinishwa tarehe 30 Septemba 2022
- Haijaanza
- [Hili ni toleo la hati hii kutoka 7 Oktoba 2022.]
Sehemu ya Kwanza – Masharti ya utangulizi
1. Jina fupi na kuanza kutumika
Sheria hii itajulikana kama Sheria ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2022 na itaanza kutumika katika tarehe ambayo Waziri atatangaza katika Gazeti la Serikali.2. Matumizi
Sheria hii itatumika Tanzania Bara.3. Tafsiri
Katika Sheria hii, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo:“afya moja” maana yake ni dhana inayotumika kuweka ushirikiano baina ya sekta zinazohusika na afya ya binadamu, wanyama na mazingira, ili kuimarisha uratibu na usimamizi katika utendaji na kupanga mikakati ya pamoja inayolenga kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na milipuko ya magonjwa na visumbufu vya mimea na mazao ikiwemo madhara ya majanga yanayovuka mipaka na yanayoweza kusambaa kwa muda mfupi, usugu wa madawa, usalama wa chakula na lishe na magonjwa yasiyo ya kuambukiza;“Divisheni” maana yake ni Divisheni yenye jukumu la usimamizi na uratibu wa Maafa iliyoko ndani ya Wizara;“eneo la Maafa” maana yake ni eneo lililotangazwa kwa mujibu wa Sheria hii kuwa eneo lenye madhara ya janga au lililopata madhara kutokana na Maafa;“janga” maana yake ni balaa au baa linalotokana na nguvu za asili au shughuli za kibinadamu ambalo linaloweza kusababisha Maafa;“Jukwaa” maana yake ni Jukwaa la Taifa la Wadau wa Usimamizi wa Maafa lililoanzishwa chini ya Sheria hii;“Katibu Mkuu” maana yake ni Katibu Mkuu wa Wizara yenye dhamana ya usimamizi wa Maafa;“Kituo” maana yake ni Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura kilichoanzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 5;“kukabiliana na Maafa” maana yake ni hatua yoyote inayochukuliwa mara tu baada ya Maafa kutokea ili kuokoa maisha, mali na mazingira, kupunguza madhara ya kiafya, kutoa huduma za kibinadamu, kuimarisha usalama wa umma au kushughulikia uharibifu unaotokana na Maafa;“kupunguza madhara” maana yake ni hatua zinazoelekezwa katika kupunguza madhara ya Maafa yanayoweza kusababishwa na tukio la janga;“kurejesha hali baada ya Maafa” maana yake ni hatua zinazosaidia kurejesha hali au kuboresha mifumo ya maisha iliyoathiriwa na Maafa kwa kujenga upya au kurejesha mifumo kwa ubora zaidi ili kuzuia au kupunguza madhara ya Maafa siku zijazo;“kuzuia Maafa” maana yake ni hatua zinazochukuliwa kuzuia hatari mpya au kupunguza hatari zilizopo kutokana na shughuli na maamuzi ya kibinadamu au nguvu za asili yasisababishe kutokea kwa Maafa;“Maafa” maana yake ni madhara yanayotokana na janga ambayo yanajumuisha uharibifu wa mfumo wa kawaida katika jamii ambao husababisha vifo, majeruhi, madhara ya kisaikolojia, upotevu au uharibifu wa mali, mifumo mbalimbali ya kiteknolojia na huduma za kiuchumi na kijamii au mazingira, ambapo jamii iliyoathirika haiwezi kukabili kwa kutumia rasilimali zake bila msaada kutoka nje ya jamii hiyo;“Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Maafa” maana yake ni mkakati ambao unaainisha hatua zitakazochukuliwa katika kuzuia na kupunguza madhara ya majanga pamoja na kujiandaa kukabili na kurejesha hali pindi Maafa yanapotokea;“Sheria” maana yake ni Sheria ya Usimamizi wa Maafa;“usimamizi wa Maafa” inajumuisha hatua zinazochukuliwa kuzuia na kupunguza madhara ya majanga, kujiandaa, kukabili na kurejesha hali endapo Maafa yanatokea kwa kuzingatia sera, sheria na miongozo;“Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana ya usimamizi wa Maafa; na“Wizara” maana yake ni Wizara yenye dhamana ya usimamizi wa Maafa.Sehemu ya Pili – Mfumo wa usimamizi na uratibu wa Maafa nchini
4. Uratibu na usimamizi wa Maafa
5. Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura
Kutakuwa na Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura chini ya Divisheni ambacho kitaunganishwa na vituo vya kisekta kitakachokuwa na jukumu la kufuatilia mwenendo wa majanga, kupokea na kuchambua taarifa za tahadhari na dharura kwa ajili ya usimamizi wa Maafa.6. Mamlaka ya Waziri
7. Kamati Elekezi ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa
8. Majukumu ya Kamati Elekezi ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa
9. Kamati ya Wataalam ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa
10. Majukumu ya Kamati ya Wataalam ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa
11. Jukwaa la Taifa la Wadau wa Usimamizi wa Maafa.
12. Majukumu ya Jukwaa la Taifa la Wadau wa Usimamizi wa Maafa
Jukwaa la Taifa la Wadau wa Usimamizi wa Maafa litakuwa na jukumu la kuishauri Kamati ya Wataalam ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa kwa kutekeleza majukumu yafuatayo—13. Kamati Elekezi ya Mkoa ya Usimamizi wa Maafa
14. Majukumu ya Kamati Elekezi ya Mkoa ya Usimamizi wa Maafa
15. Kamati ya Wataalam ya Mkoa ya Usimamizi wa Maafa
16. Majukumu ya Kamati ya Wataalam ya Mkoa ya Usimamizi wa Maafa
17. Kamati Elekezi ya Wilaya ya Usimamizi wa Maafa
18. Majukumu ya Kamati Elekezi ya Wilaya ya Usimamizi wa Maafa
19. Kamati ya Wataalam ya Jiji, Manispaa, Mji na Wilaya ya Usimamizi wa Maafa
20. Majukumu ya Kamati ya Wataalam ya Jiji, Manispaa, Mji na Wilaya ya Usimamizi wa Maafa
21. Mamlaka ya Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya
Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya kwa kuzingatia maamuzi ya Kamati Elekezi ya Mkoa au Wilaya ya Usimamizi wa Maafa, atakuwa na mamlaka ya—22. Kamati ya Kata ya Usimamizi wa Maafa
23. Majukumu ya Kamati ya Kata ya Usimamizi wa Maafa
Kamati ya Kata ya Usimamizi wa Maafa itakuwa na jukumu la—24. Kamati ya Kijiji ya Usimamizi wa Maafa
25. Kamati ya Mtaa ya Usimamizi wa Maafa
26. Majukumu ya Kamati ya Kijiji au Mtaa ya Usimamizi wa Maafa
Kamati ya Kijiji au Mtaa ya Usimamizi wa Maafa itakuwa na jukumu la—27. Utoaji taarifa za Usimamizi wa Maafa
28. Miongozo ya Kamati za Maafa
29. Kanuni za Kamati
Kamati zilizoanzishwa chini ya Sheria hii zitaandaa taratibu za uendeshaji wa shughuli zake katika mamlaka husika.Sehemu ya Tatu – Mkakati wa taifa wa Taifa wa Usimamizi wa Maafa na operesheni wakati wa Maafa
30. Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Maafa
31. Wajibu wa jumla
32. Kutangaza eneo la Maafa
33. Maafa yanayoashiria hali ya hatari
Sehemu ya Nne – Mfuko wa Taifa wa Usimamizi wa Maafa
34. Mfuko wa Taifa wa Usimamizi wa Maafa
35. Usimamizi wa makusanyo na misaada
Sehemu ya Tano – Masharti ya jumla
36. Makosa na adhabu
37. Makosa yanayosababishwa na taasisi
Endapo kosa limetendwa chini ya sheria hii na taasisi au kampuni, mtu yeyote ambaye wakati kosa hilo linatendwa alihusika na usimamizi wa taasisi au kampuni hiyo atachukuliwa kuwa yeye ndiye aliyetenda kosa hilo, isipokuwa kama ataithibitishia mahakama kuwa hakufahamu na katika mazingira ya kawaida asingeweza kufahamu kuhusu kutendeka kwa kosa hilo.38. Adhabu ya jumla
Mtu yeyote anayekiuka masharti yoyote ya Sheria hii, na iwapo hakuna adhabu mahsusi iliyotamkwa, atakuwa anatenda kosa, na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi laki tatu na isiyozidi shilingi milioni tano au kifungo kisichopungua mwezi mmoja na kisichozidi mwaka mmoja au vyote.39. Kinga dhidi ya mashtaka
Mtu yeyote ambaye kwa mujibu wa Sheria hii au kanuni ameruhusiwa kushiriki katika utekelezaji wa masharti ya Sheria hii hatashtakiwa binafsi kwa jambo lolote alilolitenda au kuacha kutenda kwa nia njema wakati akitekeleza shughuli yoyote ya usimamizi wa Maafa.40. Kanuni
Waziri atatengeneza Kanuni kuhusu suala lolote ambalo ni la lazima kwa madhumuni ya utekelezaji wa Sheria hii.41. Kufutwa na masharti ya mwendelezo
History of this document
07 October 2022 this version
30 September 2022
Assented to
Subsidiary legislation
Title
|
|
---|---|
Government Notice 658A of 2022 |