Tanzania
Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ya Mwaka, 2023
Tenda 13 ya 2023
- Imechapishwa katika Tanzania Government Gazette 48 hadi 1 Disemba 2023
- Imeidhinishwa tarehe 19 Novemba 2023
- Imeanza
- [Hili ni toleo la hati hii kama ilivyokuwa kutoka 1 Disemba 2023 hadi 30 Juni 2024.]
Sehemu ya kwanza – Masharti ya utangulizi
1. Jina na kuanza kutumika
2. Matumizi
Sheria hii itatumika Tanzania Bara.3. Definitions
Katika Sheria hii, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo—“Benki” maana yake ni Benki Kuu ya Tanzania iliyoanzishwa kwa Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania;[Sura ya 197]“bima ya afya kwa wote” maana yake ni utaratibu ulioidhinishwa kwa mujibu wa Sheria hii unaowezesha kila mwananchi kupata huduma za afya kupitia bima ya afya bila kikwazo cha fedha pindi anapozihitaji huduma hizo;“Divisheni” ina maana kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Hifadhi ya Jamii;[Sura ya 135]“kitita cha bima ya afya cha jamii” maana yake ni kitita cha mafao kilichoanzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 15;“kitita cha huduma za ziada” maana yake ni kitita cha huduma za afya zaidi ya kitita cha mafao ya huduma muhimu kinachotolewa na skimu ya bima ya afya;“kitita cha mafao” maana yake ni huduma za afya zinazotolewa kwa mnufaika wa skimu ya bima ya afya;“kitita cha mafao ya huduma muhimu” maana yake ni kitita cha mafao kilicho anzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 14;“kitita maalum cha mafao” maana yake ni kitita cha mafao kitakachoanzishwa chini ya kifungu cha 8(2);“kituo cha huduma za afya” inajumuisha kliniki, zahanati, kituo cha afya, hospitali, maabara, duka la dawa au kituo kingine chochote kinachotoa huduma za afya;“kituo cha huduma za afya kilichoingia mkataba” maana yake kituo cha kutolea huduma za afya kilichoingia makubaliano na skimu kuwahudumia wanufaika kwa mujibu wa Sheria hii;“kiwango cha mchango” maana yake ni kiwango kutoka katika mshahara au chanzo kingine chochote kitakacholipwa katika skimu ya bima ya afya na mwanachama au kwa niaba ya mwanachama;“kiwango cha uchangiaji” maana yake ni kiasi cha fedha kinacholipwa kwa lengo la kuwa mwanachama kwa mujibu wa Sheria hii;“Mamlaka” maana yake ni Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania iliyoanzishwa kwa Sheria ya Bima;[Sura ya 394]“mkazi” ina maana kama ilivyotafsiriwa katika Sheria ya Uhamiaji;[Sura ya 54]“mnufaika” maana yake ni mtu anayestahili kupata mafao ya matibabu chini ya Sheria hii;“mshahara” kwa madhumuni ya:(a)mtumishi wa umma, maana yake ni mshahara usiojumuisha malipo ya ziada, stahiki, na posho;(b)mwajiriwa wa sekta binafsi, maana yake ni mshahara unaojumuisha stahiki zote za kisheria zinazolipwa kama sehemu ya mshahara wa mwajiriwa;“mtegemezi” maana yake ni—(a)mzazi wa mwanachama au mzazi wa mwenza wa mwanachama;(b)mtoto wa mwanachama wa kuzaa, kuasili au wa kambo aliye na umri chini ya miaka ishirini na moja; au(c)ndugu wa damu wa mwanachama aliye na umri wa chini ya miaka ishirini na moja;“mtoa huduma” inajumuisha kituo cha kutolea huduma za afya na skimu ya bima ya afya chini ya Sheria hii.“mtu aliyejiajiri” maana yake ni mtu anayefanya kazi asiye katika uhusiano wa mwajiri na mwajiriwa;“mtu asiye na uwezo” maana yake ni mtu anayeishi kwa kipato kilicho chini ya mstari unaopima kiwango cha umaskini kama inavyofafanuliwa na mamlaka husika;“mwajiri” ina maana kama ilivyotafsiriwa katika Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini;[Sura ya 366]“mwajiriwa” ina maana kama ilivyotafsiriwa katika Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini;[Sura ya 366]“mwanachama” maana yake ni mtu yeyote aliyesajiliwa katika skimu chini ya Sheria hii na anachangia ama yeye mwenyewe au kupitia kwa Serikali;[Sura ya 366]“ndugu wa damu” maana yake ni kaka au dada wa kuzaliwa wa mwanachama na aliye chini ya umri wa miaka ishirini na moja;“raia” ina maana kama ilivyotafsiriwa katika Sheria ya Uraia;“sekta isiyo rasmi” maana yake ni sekta inayojumuisha wafanyakazi wanaofanya kazi zisizo rasmi na ambao hawana mikataba ya ajira au mikataba mingine yoyote iliyoelezewa katika tafsiri ya neno “mwajiriwa” na inajumuisha mtu asiyejihusisha na aina yoyote ya uzalishaji;“sekta rasmi” maana yake ni sekta inayojumuisha kazi zilizorasimishwa na kufanywa kwa mikataba ambapo mikataba hiyo imeainisha mishahara au ujira na muda maalum wa kazi;“sekta rasmi binafsi” inajumuisha wafanyakazi katika mashirika au taasisi isipokuwa watumishi wa sekta ya umma;“sekta ya umma” maana yake ni sekta inayojumuisha watumishi wa umma pamoja na wafanyakazi katika mashirika au taasisi binafsi ambayo Serikali inamiliki angalau asilimia thelathini ya hisa;“skimu ya bima ya afya” maana yake ni bima ya afya ya umma au kampuni binafsi inayotoa huduma za bima ya afya chini ya Sheria hii;“skimu ya bima ya afya binafsi” maana yake ni bima ya afya iliyoanzishwa au kutambuliwa chini ya Sheria hii;“skimu ya bima ya afya ya umma” maana yake ni bima ya afya iliyoanzishwa au kutambuliwa chini ya Sheria hii;“Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana na masuala ya afya; na“Wizara” maana yake ni Wizara yenye dhamana ya masuala ya afya.4. Malengo
Malengo ya Sheria hii yatakuwa—Sehemu ya pili – Mfumo wa bima ya afya kwa wote
5. Ulazima wa bima ya afya
6. Mfumo wa bima ya afya
Mfumo wa bima ya afya kwa wote utajumuisha—7. Udhibiti wa mfumo wa bima ya afya
Sehemu ya tatu – Skimu za bima ya afya
8. Skimu ya bima ya afya ya umma
9. Skimu ya bima ya afya binafsi
10. Zuio la kuendesha skimu ya bima ya afya
11. Utunzaji wa rejesta
Mamlaka itatunza rejesta ya skimu za bima ya afya zilizosajiliwa kwa mujibu wa Sheria hii na skimu nyingine za bima ya afya zilizokuwepo kabla ya kuanza kutumika kwa Sheria hii.12. Kufuta usajili wa skimu ya bima ya afya
Sehemu ya nne – Vitita vya mafao
(a) – Kitita cha mafao ya huduma muhimu
13. Kitita cha mafao ya huduma muhimu
14. Huduma za kitita cha mafao ya huduma muhimu
(b) – Kitita cha bima ya afya cha jamii
15. Kitita cha bima ya afya cha jamii
16. Akaunti ya kitita cha bima ya afya cha jamii
17. Usimamizi na uendeshaji wa kitita cha bima ya afya cha jamii
Waziri, kwa kushauriana na Waziri mwenye dhamana na masuala ya serikali za mitaa, anaweza kutunga kanuni kwa ajili ya kuweka utaratibu wa usimamizi na uendeshaji wa kitita cha bima ya afya cha jamii.(c) – Kitita cha huduma za ziada
18. Kitita cha huduma za ziada
Sehemu ya tano – Uanachama na uchangiaji katika skimu ya bima ya afya
19. Uanachama
20. Wanufaika
Mwanachama anaweza kusajili watu wafuatao kama wanufaika:21. Wigo wa upatikanaji wa huduma za afya
Mwanachama au mnufaika anaweza kupata huduma za afya mahala popote katika kituo cha kutolea huduma za afya kilichoingia mkataba na skimu ya bima ya afya kwa ajili ya utoaji wa huduma za afya kwa kuzingatia miongozo ya Wizara ikiwemo miongozo ya rufaa.22. Usajili wa wanachama katika skimu ya bima ya afya
23. Viwango vya uchangiaji
24. Utambuzi na upatikanaji wa huduma kwa watu wasio na uwezo
25. Mfuko wa kugharamia wasio na uwezo, nk.
26. Uwekaji wa amana
27. Utambuzi wa uanachama
Skimu ya bima ya afya itaweka utaratibu kwa ajili ya—28. Ukomo wa uanachama
Sehemu ya sita – Udhibiti ubora
29. Viwango vya udhibiti ubora vya skimu ya bima ya afya
Skimu ya bima ya afya itatekeleza viwango vya ubora vitakavyoainishwa na Mamlaka.30. Udhibiti ubora wa watoa huduma za afya
Wizara itakuwa na jukumu la kuhakikisha kuwa vituo vya kutolea huduma vilivyoingia mikataba na skimu za bima ya afya vinatekeleza viwango vya ubora vilivyotolewa na Wizara au kwa mujibu wa Sheria.Sehemu ya saba – Masharti mengineyo
31. Ukwasi na uendelevu wa bima ya afya
32. Uwekezaji wa skimu za bima ya afya
33. Gharama za usimamizi na uendeshaji
Mamlaka itatoa miongozo kuhusu ukomo wa juu wa gharama za uendeshaji wa skimu ya bima ya afya.34. Malalamiko na usuluhishi wa migogoro
Utaratibu wa kushughulikia malalamiko na utatuzi wa migogoro baina ya au dhidi ya skimu ya bima ya afya, kituo cha huduma za afya kilichoingia mkataba, mnufaika, mwajiri na mtu yeyote anayehusika utakua kama ulivyoainishwa kwenye Sheria ya Bima.[Sura ya 394]35. Mamlaka ya kutunga kanuni
Waziri anaweza kutengeneza kanuni zitakazoainisha—36. Taarifa za uongo
37. Kutojiunga na skimu ya bima ya afya
38. Utaratibu wa madai ya skimu ya bima ya afya
39. Makosa ya jumla
Mtu anayekiuka masharti yoyote ya Sheria hii pale ambapo hakuna adhabu mahususi iliyowekwa, anatenda kosa na akitiwa hatiani, atawajibika—40. Makosa yatendwayo na taasisi
Endapo kosa limetendwa na kampuni au taasisi chini ya Sheria hii, mkurugenzi, meneja au mbia wa kampuni au taasisi hiyo atawajibika, ikiwa atatiwa hatiani, kwa adhabu iliyoainishwa kuhusiana na kosa hilo, isipokuwa kama mkurugenzi, meneja au mbia huyo ataithibitishia mahakama kwa kiasi cha kuiridhisha kwamba kitendo kilichosababisha kosa hilo kufanyika kilifanyika pasipo yeye kuwa na uelewa, kutoa idhini au kuchukua hatua za makusudi kuzuia kosa hilo kutendeka.41. Mkinzano na sheria nyingine
Endapo kutakuwa na mkinzano baina ya masharti ya Sheria hii na masharti ya sheria nyingine yoyote kuhusiana na masuala ya bima ya afya, masharti ya Sheria hii yatapewa kipaumbele.Sehemu ya nane – Kufutwa kwa sheria na masharti ya mpito
42. Kufutwa kwa sheria na masharti yanayoendelea
43. Masharti ya mpito
Sehemu ya tisa – Marekebisho ya sheria mbalimbali
(a) – Sheria ya fuko wa ta.fa wa bima ya afya
[Sura ya 395]44. Ufafanuzi
Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”.[Sura ya 395]45. Marekebisho ya kifungu cha 2
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 2(1) kwa kuongeza maneno “persons under formal private sector, students” kati ya maneno “Councillors,” na “retirees”.46. Marekebisho ya kifungu cha 3
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 3 kwa kufuta tafsiri ya neno “Authority” na badala yake kuweka tafsiri ifuatayo:47. Marekebisho ya kifungu cha 11
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu 11(1) kwa kuongeza maneno “persons under formal private sector, student and children” baada ya neno “Councilors” lililopo katika aya (e).48. kufutwa na kuandikwa upya kwa kifungu cha 16
Sheria Kuu inarekebishwa kwa kufuta kifungu cha 16 na badala yake kuweka kifungu kifuatacho:49. Kufutwa na kuandikwa upya kwa kifungu cha 40
Sheria Kuu inarekebishwa kwa kufuta kifungu cha 40 na badala yake kuweka kifungu kifuatacho:50. Kufutwa kwa vifungu vya 41 na 42
Sheria ya Kuu inarekebishwa kwa kufuta vifungu vya 41 na 42(b) – Sheria ya hfadhi ya jamii
[Sura ya 135]51. Ufafanuzi
Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Hifadhi ya Jamii ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”.[Sura ya 135]52. Marekebisho ya kifungu cha 61
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 61(b)(ii) kwa kufuta maneno “Ministry responsible for health matters” na badala yake kuweka maneno “Tanzania Insurance Regulatory Authority pursuant to the Universal Health Insurance Act.”(c) – Sheria ya bima
[Sura ya 394]53. Ufafanuzi
Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Bima ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”.[Sura ya 394]54. Marekebisho ya kifungu cha 6
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 6—55. Marekebisho ya kifungu cha 123
Sheria Kuu inarekebishwa kwa—56. Marekebisho ya kifungu cha 124
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 124 kwa kuongeza mara baada ya kifungu kidogo cha (4), kifungu kidogo cha (5) kama ifuatavyo:57. Marekebisho ya kifungu cha 126
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 126 kwa kufuta na kuandika upya kifungu kidogo cha (2) kama ifuatavyo—(d) – Sheria ya fuko wa ta.fawahfadhi ya jamii
[Sura ya 50]58. Ufafanuzi
Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii, ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”.[Sura ya 50]59. Marekebisho ya kifungu cha 21
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 21(1) kwa kufuta neno “insurance” lililopo katika aya (g).60. Kufutwa na kuandikwa upya kifungu cha 41
Sheria Kuu inarekebishwa kwa kufuta kifungu cha 41 na kukiandika upya kama ifuatavyo:61. Marekebisho ya kifungu cha 42
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 42(1) kwa kufuta maneno “based on health insurance”.(e) – Sheria ya mtoto
[Sura ya 13]62. Ufafanuzi
Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Mtoto ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”.[Sura ya 13]63. Marekebisho ya kifungu cha 8
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 8 kwa kuongeza kifungu kidogo cha (7) kama ifuatavyo:(f) – Sheria ya ajira na mahusiano kazini
[Sura ya 366]64. Ufafanuzi
Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”.[Sura ya 366]65. Kuongezwa kwa sehemu ndogo E
Sheria Kuu inarekebishwa kwa kuongeza mara baada ya kifungu cha 11 Sehemu Ndogo ya E kama ifuatavyo—(g) – Sheriaya udhibiti wa hospitali bincfsi
[Sura ya 151]66. Ufafanuzi
Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Udhibiti wa Hospitali Binafsi ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”.[Sura ya 151]67. Marekebisho ya kifungu cha 7
Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 7(2)—(a) kwa kuongeza mara baada ya aya (b), aya ifuatayo—(b) kwa kubadilisha mpangilio wa aya (c) kuwa aya (d); na(c) katika aya (d) kama ilivyobadilishwa, kwa kufuta neno “five” na badala yake kuweka neno “four”.History of this document
01 July 2024 amendment not yet applied
Amended by
Finance Act, 2024
01 December 2023 this version
19 November 2023
Assented to