Tanzania
Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ya Mwaka 2024
Tenda 2 ya 2024
- Imechapishwa katika Gazette of the United Republic of Tanzania 12 hadi 22 Machi 2024
- Imeidhinishwa tarehe 7 Machi 2024
- Ilianza 12 Aprili 2024 kwa Notisi ya Tarehe ya Kuanza Kutumika kwa Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ya Mwaka, 2024
- [Hili ni toleo la hati hii kutoka 22 Machi 2024.]
Sehemu ya Kwanza – Masharti ya utanguliz
1. Jina na tarehe ya kuanza kutumika
Sheria hii itajulikana kama Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ya mwaka 2024 na itaanza kutumika katika tarehe ambayo Waziri atateua kwa notisi katika Gazeti la Serikali.2. Matumizi
Sheria hii itatumika Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar, isipokuwa kwa masuala yanayohusu uchaguzi wa Madiwani, itatumika Tanzania Bara.3. Tafsiri
Katika Sheria hii, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo—"jimbo" maana yake ni jimbo la uchaguzi kwa madhumuni ya uchaguzi wa Wabunge;"Katiba" maana yake ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977;"Mjumbe" maana yake ni mtu aliyeteuliwa kuwa mjumbe wa Tume kwa mujibu wa Ibara ya 74 ya Katiba;"Mkurugenzi wa Uchaguzi" maana yake ni mtu aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 17 na itajumuisha mtu ambaye kwa kipindi hicho atakuwa anatekeleza majukumu yoyote ya ofisi hiyo;"Mwenyekiti" maana yake ni mtu aliyeteuliwa kuongoza Tume na inajumuisha Makamu Mwenyekiti;"Rais" maana yake ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;"Tume" maana yake ni Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi iliyoanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 74(1) ya Katiba;"uchaguzi" maana yake ni uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani na inajumuisha uchaguzi mdogo wa Mbunge au Diwani;"Waziri" maana yake ni Waziri mwenye dhamana na masuala ya uchaguzi.Sehemu ya Pili – Kuanzishwa, muundo na majukumu ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi
4. Kuanzishwa kwa Tume
Kutakuwa na Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano iliyoanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 74(1) ya Katiba ambayo pia itajulikana kama “Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi”.5. Muundo wa Tume
6. Hadhi ya Tume
7. Sifa za wajumbe wa Tume
8. Muda wa utumishi wa wajumbe
9. Kamati ya Usaili
10. Majukumu ya Tume
11. Maadili katika utendaji kwa wajumbe
Kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu ya Tume, kila Mjumbe wa Tume atalazimika kuzingatia Sheria ya Kanuni za Maadili ya Viongozi wa Umma na Kanuni za Maadili zitakazoandaliwa chini ya Sheria hii.[Sura ya 398]12. Vikao vya Tume
13. Akidi katika vikao vya Tume
Akidi ya kikao chochote cha Tume itakuwa si chini ya wajumbe wanne.14. Uamuzi wa Tume
15. Posho na stahili za wajumbe wa Tume
16. Uhusiano kati ya Tume na Tume ya uchaguzi ya Zanzibar
Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 74(13) ya Katiba, katika utekelezaji wa majukumu yake, Tume itashauriana mara kwa mara na Tume ya Uchaguzi ya Tanzania Zanzibar.Sehemu ya Tatu – Sekretarieti ya Tume huru ya taifa ya uchaguzi
17. Mkurugenzi wa Uchaguzi
18. Maadili ya utendaji kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi
Mkurugenzi wa Uchaguzi ataapa mbele ya Rais kabla ya kuanza kutekeleza majukumu yake na atalazimika kuzingatia Sheria ya Kanuni za Maadili ya Viongozi wa Umma na Kanuni za Maadili zitakazoandaliwa chini ya Sheria hii.[Sura ya 398]19. Majukumu ya Mkurugenzi wa Uchaguzi
20. Watumishi na watendaji wa Tume
Sehemu ya Nne – Masharti ya fedha
21. Fedha za uendeshaji wa Tume
Fedha za "uendeshaji wa shughuli za Tume zitatoka katika bajeti ya Serikali.22. Gharama kulipwa kutoka mfuko mkuu wa hazina ya serikali
Gharama zote—23. Hesabu na ukaguzi
24. Taarifa ya mwaka
Sehemu ya Tano – Masharti mengineyo
25. Muundo wa utumishi wa Sekretarieti ya Tume
Tume kwa kushauriana na Waziri mwenye dhamana na masuala ya utumishi, itaandaa Muundo wa Utumishi wa Sekretarieti ya Tume.26. Kanuni na miongozo
Tume inaweza kutengeneza kanuni na miongozo na kutoa maelekezo kwa ajili ya utekelezaji bora wa majukumu yake.27. Masharti ya mpito
Mara baada ya kuanza kutumika kwa Sheria hii, mtu yeyote ambaye ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti au Mjumbe wa Tume ataendelea kushika madaraka hayo hadi pale ujumbe wake utakapokoma.History of this document
12 April 2024
22 March 2024 this version
07 March 2024
Assented to
Cited documents 0
Subsidiary legislation
Title
|
|
---|---|
Legislation
|
Government Notice 390 of 2024 |