Tanzania
Sheria ya Shirika la Utangazaji Tanzania ya Mwaka, 2025
Tenda 3 ya 2025
- Imechapishwa katika Special Gazette of the United Republic of Tanzania 3 hadi 14 Machi 2025
- Imeidhinishwa tarehe 4 Machi 2024
- Haijaanza
- [Hili ni toleo la hati hii kutoka 14 Machi 2025.]
Sehemu ya Kwanza – Masharti ya utangulizi
1. Jina na kuanza kutumika
Sheria hii itajulikana kama Sheria ya Shirika la Utangazaji Tanzania ya Mwaka 2025 na itaanza kutumika tarehe ambayo Waziri atateua kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali.2. Tafsiri
Katika Sheria hii, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo:—“Bodi” maana yake ni Bodi ya Wakurugenzi iliyoanzishwa chini ya kifungu cha 6;“chaneli maalumu” inajumuisha chaneli, idhaa, kituo au jukwaa lililoanzishwa na Serikali kwa madhumuni mahsusi, linalosimamiwa na kuendeshwa na Shirika;“huduma ya utangazaji ya kulipia” maana yake ni huduma ya utangazaji ambayo inaweza kupatikana kwa mtu kwa malipo ya ada;“huduma ya utangazaji wa umma” maana yake ni aina ya huduma ya utangazaji ambayo inatolewa kwa umma, inayofadhiliwa na umma na haina faida ya kibiashara;“kipindi maalumu” maana yake ni kipindi chenye maslahi ya umma ambacho kinaweza kutangazwa wakati wowote katika kutimiza wajibu wa Shirika kwa umma na bila kujali kuwa kuna vipindi vingine katika ratiba;“matukio ya kitaifa” maana yake ni ziara za Viongozi Wakuu wa Serikali, sherehe za kitaifa, maadhimisho, matukio au kumbukumbu mbalimbali za kitaifa;“miundombinu ya utangazaji” maana yake ni miundombinu ya usambazaji wa maudhui ya utangazaji na inajumuisha mifumo ya utangazaji, studio, vifaa vya kurushia matangazo, mitambo, ardhi na majengo yanayotumika kuhifadhi miundombinu hiyo;“mjumbe” maana yake ni mjumbe wa Bodi na inajumuisha Mwenyekiti;“Mkurugenzi Mkuu” maana yake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika aliyeteuliwa chini ya kifungu cha 12;“mtumishi” maana yake ni mtumishi yeyote wa Shirika na inajumuisha Mkurugenzi Mkuu;“Shirika” maana yake ni Shirika la Utangazaji Tanzania ambalo limetambuliwa chini ya kifungu cha 3;“tangazo la biashara” maana yake ni tangazo lolote kwa umma lenye madhumuni ya kukuza uuzaji, ununuzi au ukodishaji wa bidhaa au huduma, lililotengewa muda wa kutangazwa kwa malipo ya fedha au malipo mengine lenye madhumuni ya kuhamasisha kusudi au wazo au kuleta manufaa mengine anayotamani mtoa tangazo;“udhamini” maana yake ni ushiriki wa mtu ambaye hajishughulishi katika shughuli za utangazaji au utayarishaji wa kazi za maudhui katika ufadhili wa moja kwa moja au usio wa moja kwa moja wa vipindi kwa nia ya kukuza jina, alama ya biashara au taswira ya mtu huyo;“Viongozi Wakuu wa Serikali” maana yake ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Makamu wa Rais, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Waziri Mkuu; na“Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana ya huduma za utangazaji.Sehemu ya Pili – Shirika la utangazaji Tanzania
3. Kuendelea kutambulika kwa Shirika
4. Majukumu na mamlaka ya Shirika
Majukumu na mamlaka ya Shirika yatakuwa—5. Wajibu wa Shirika katika kuandaa vipindi
Katika kutekeleza majukumu yake, Shirika litaandaa vipindi—Sehemu ya Tatu – Utawala na usimamizi wa shirika
6. Bodi ya Shirika
7. Sifa za kuwa mjumbe
Mtu atakuwa na sifa za kuteuliwa kuwa mjumbe wa Bodi iwapo mtu huyo—8. Majukumu na mamlaka ya Bodi
9. Mamlaka ya ukasimishaji
10. Ada au posho za wajumbe wa Bodi
Mjumbe atalipwa na Shirika ada au posho kama itakavyoamuliwa na Bodi na kuidhinishwa na mamlaka husika.11. Kinga kwa wajumbe wa Bodi
Mjumbe wa Bodi hatachukuliwa hatua au kufunguliwa shauri kuhusiana na kitendo au jambo lolote alilotenda au kuacha kutenda kwa nia njema katika kutekeleza majukumu yake chini ya Sheria hii.12. Mkurugenzi Mkuu
13. Majukumu ya Mkurungenzi Mkuu
Pamoja na majukumu mengine aliyopewa kwa mujibu wa Sheria hii, Mkurugenzi Mkuu atakuwa na majukumu ya—14. Watumishi wa Shirika
Sehemu ya Nne – Miundombinu ya Shirika
15. Miundombinu ya utangajazi
16. Ulinzi na usimamizi wa miundombinu ya utangajazi
Shirika litasimamia miundombinu katika namna inayohakikisha manufaa ya kiusalama, kiuchumi na kibiashara katika miundombinu ya utangazaji.Sehemu ya Tano – Makatazo
17. Uharibifu wa mali za Shirika
18. Kuingia kwenye eneo la Shirika
Mtu ambaye—19. Matumizi ya maudhui
Sehemu ya Sita – Masharti ya fedha
20. Vyanzo vya fedha vya Shirika
21. Usimamizi wa fedha
Fedha za Shirika zitasimamiwa na Bodi kwa mujibu wa sheria na kanuni za fedha na zitatumika kulipia gharama zinazohusiana na utendaji wa majukumu ya Shirika chini ya Sheria hii.22. Makadirio ya mapato na matumizi
23. Matumizi ya fedha
24. Hesabu na ukaguzi
25. Taarifa ya mwaka
Sehemu ya Saba – Masharti ya jumla
26. Udhamini wa vipindi
Kipindi chochote au kipindi maalumu kinachotangazwa na Shirika au kwa niaba ya Shirika kinaweza kudhaminiwa na kujumuisha matangazo ya biashara.27. Matengenezo au mabadiliko yanayoweza kuharibu mfumo wa matangazo
28. Uanzishwaji wa chaneli maalumu
29. Adhabu ya jumla
Mtu anayetenda kosa chini ya Sheria hii na hakuna adhabu mahsusi iliyoainishwa, akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi milioni tano na isiyozidi shilingi milioni kumi au kifungo kisichopungua miaka miwili na kisichozidi miaka mitano au vyote.30. Mamlaka ya Waziri kutengeneza kanuni
31. Masharti ya mwendelezo
Mambo yote yaliyofanyika kwa mujibu wa Amri ya Uanzishwaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania ya Mwaka 2007, yataendelea kuwa halali na yatatafsiriwa kuwa yalifanyika chini ya Sheria hii.[TS. Na. 186 la 2007]History of this document
14 March 2025 this version
04 March 2024
Assented to