This is the latest version of this Government Notice.
Tanzania
Land Disputes Courts Act, 2002
Kanuni za Uteuzi, Malipo na Nidhamu kwa Madalali wa Mabaraza na Wasambaza Nyaraka za Mwaka 2024
Tangazo la Serikali 172 ya 2023
- Imechapishwa katika Government Gazette kwa 17 Machi 2023
- Imeidhinishwa tarehe 6 Machi 2023
- Ilianza tarehe 17 Machi 2023
- [Hili ni toleo la hati hii kutoka 26 Januari 2024.]
- [Iliyorekebishwa na Kanuni za Marekebisho ya Kanuni za Uteuzi, Malipo na Nidhamu kwa Madalali wa Baraza na Wasambaza Nyaraka za Mwaka 2024 (Tangazo la Serikali 61 ya 2024) hadi 26 Januari 2024]
Sehemu ya Kwanza – Masharti ya utangulizi
1. Jina
Kanuni hizi zitajulikana kama Kanuni za Uteuzi, Malipo na Nidhamu za Madalali wa Mabaraza na Wasambaza Nyaraka za Mwaka 2023.2. Tafsiri
Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo—“Afisa Masuhuli” maana yake ni Katibu Mkuu wa Wizara yenye dhamana na masuala ya Ardhi;“afisa mtekelezaji” maana yake ni dalali wa Baraza, msambaza nyaraka au mtu mwingine yeyote anayeteuliwa na Mwenyekiti kutekeleza kibali cha kushikilia au amri ya Baraza ikiwa ni pamoja na kuuza, kuondolewa, kubomoa aukusambaza nyaraka za Baraza;“Baraza” maana yake ni Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya kama ilivyotamkwa katika Sheria;“dalali wa Baraza” maana yake ni mtu aliyeteuliwa chini ya kanuni ya 6 ya Kanuni hizi;“Kamati” maana yake ni Kamati Ndogo iliyoundwa chini ya kifungu cha 28B cha Sheria;“Kamati Ndogo” maana yake ni Kamati iliyoundwa chini ya kanuni ya 4(1)(c) ya Kanuni hizi;“Kanuni za Maadili” maana yake ni Kanuni za Maadili zinazorejewa chini ya kanuni ya 1 ya Kanuni hizi;“Katibu” maana yake ni Katibu wa Kamati;“kukosa uwezo” maana yake ni udhaifu wa mwili au akili uliothibitishwa na daktari anayetambulika na Bodi ya Madaktari;[definition of "kukosa uwezo" inserted by section 2 of Government Notice 61 of 2024]“Msajili” maana yake ni Msajili wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya aliyeteuliwa chini ya kifungu cha 28(1) cha Sheria na inamjumuisha Msajili Msaidizi;“msambaza nyaraka” maana yake ni mtu aliyeteuliwa chini ya kanuni ya 6(2) au anayehusika chini ya masharti ya Kanuni hizi kusambaza nyaraka za Baraza;“nyaraka za Baraza” maana yake ni nyaraka za kisheria zinazotolewa na Baraza kwa ajili ya huduma kwa wahusika;“siku za kazi” maana yake ni Jumatatu hadi Ijumaa na haijumuishi sikukuu za umma;“Sheria” maana yake ni Sheria ya Mahakama za Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi;[Sura ya 216]“tovuti” maana yake ni tovuti rasmi ya Wizara inayohusika na ardhi; na“Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana na ardhi;Sehemu ya Pili – Uteuzi wa madalali wa baraza na wasambaza nyaraka
3. Uteuzi, muundo, muda wa kukaa madarakani
4. Majukumu ya Kamati
5. Majukumu ya Kamati Ndogo
Majukumu ya Kamati Ndogo yatakuwa ni—6. Uteuzi na sifa za kuteuliwa kuwa dalali wa Baraza au msambaza nyaraka
7. Maombi ya kuteuliwa kuwa dalali au msambaza nyaraka
8. Wajibu na kazi za dalali wa Baraza
Kazi kuu ya dalali wa Baraza itakuwa ni kutekeleza tuzo au amri za mabaraza zilizo chini ya mamlaka yake na itajumuisha majukumu yafuatayo:9. Wajibu na kazi za msambaza nyaraka
Kazi za msambaza nyaraka zitakuwa kupeleka wito na zitajumuisha kupeleka—10. Akau nti ya Baraza
Afisa Masuhuli au mtu yeyote aliyeidhinishwa atafungua na kutunza akaunti maalum ya benki ambayo fedha zote zilizolipwa katika utekelezaji wa amri, na tuzo za Baraza zitawekwa.11. Mwenendo wa dalali au msambaza nyaraka
Kila dalali na msambaza nyaraka atatii masharti ya Kanuni hizi, Kanuni za Maadili zilizoainishwa katika Jedwali la Pili na Jedwali la Tatu la Kanuni hizi mtawalia, amri za Baraza, Msajili au Kamati.12. Ripoti ya utendaji kazi
13. Uhuishaji wa cheti
14. Sababu za kukataa kuhuisha cheti cha dalali au msambaza nyaraka
Sehemu ya Tatu – Hatua za kinidhamu
15. Hatua za kinidhamu
Kamati inaweza kuanzisha mashauri ya kinidhamu dhidi ya dalali au msambaza nyaraka katika mazingira yafuatayo:16. Malalamiko dhidi ya dalali au masambaza nyaraka
Malalamiko yoyote dhidi ya dalali au msambaza nyaraka yatawasilishwa kwa Katibu au Msajili Msaidizi ambaye kwa madhumuni ya Kanuni hii atatambulika kama Katibu wa Kamati Ndogo.17. Ushughulikiaji wa malalamiko
18. Kusimamish wa kwa dalali au msambaza nyaraka
19. Mwenendo wa mashauri ya kinidhamu
20. Athari za ubatilishaji au kufungiwa kwa cheti
Endapo cheti kimefungiwa, kufutwa au hakijahuishwa—21. Rufaa
Endapo dalali au msambaza nyaraka hajaridhika na uamuzi wa Kamati, anaweza kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo Mahakama Kuu ndani ya siku arobaini na tano tangu tarehe ya uamuzi.Sehemu ya Nne – Utekelezaji wa tuzo na amri
22. Daftari la utekelezaji hukumu
Baraza na dalali wataweka na kutunza daftari la utekelezaji wa hukumu zote lenye maelezo kama ilivyoainishwa katika Jedwali la Kwanza la Kanuni hizi—23. Notisi kwa mdaiwa tuzo
24. Mdaiwa tuzo kutii amri
Endapo mdaiwa tuzo anatekeleza amri au anatii amri ya Baraza na kulipa gharama alizotumia dalali kama ilivyokadiriwa na kutozwa na Mwenyekiti ndani ya muda uliotolewa na dalali chini ya Kanuni hizi, hati au amri hiyo itakoma kuwa na nguvu ya kisheria.25. Thamani ya mali inayoweza kukamatwa
Afisa mtekelezaji hukumu, hatakamata mali ambayo thamani yake ya bei ya soko inazidi kiwango kilichobainishwa katika tuzo na gharama za utekelezaji wa hukumu kwa mujibu wa Kanuni hizi, isipokuwa ikiwa imeamuliwa na Baraza.26. Uwasilishaji wa orodha thamani yake
27. Kuhifadhi fedha za utekelezaji
28. Tozo na amana wakati wa kukamata mali na amri ya kuuza
Sehemu ya Tano – Ada na gharama
29. Ada na tozo ya madalali
30. Gharama za kukamata mali, na gharama nyinginezo
31. Uwasilishaji wa gharama za kesi kwa Baraza
Dalali, ndani ya muda usiozidi siku thelathini tangu tarehe ya mwisho ya kusikilizwa kwa maombi ya kukazia hukumu, atawasilisha gharama za kesi katika Baraza lililotoa amri ya utekelezaji wa hukumu na kuwasilisha nakala za gharama hizo kwa pande zote za shauri, na Baraza ndani ya siku kumi na nne litaamua kiasi cha gharama ambacho kinapaswa kulipwa baada ya kusikiliza pande zote.32. Mapato yaliyotokana na utekelezaji wa hukumu
Baraza lililotoa amri ya utekelezaji wa hukumu litatumia mapato ya utekelezaji hukumu yaliyowekwa kwenye akaunti ya Baraza kwa—33. Masharti maalum kuhusu mifugo
34. Ada na gharama za msambaza nyaraka
35. Afisa wa umma aliyeteuliwa kama dalali au msambaza nyaraka
Endapo afisa wa umma amepewa jukumu la kutekeleza majukumu ya dalali au msambaza nyaraka, ada na gharama zilizoainishwa katika Jedwali la Nne na Jedwali la Tano la Kanuni hizi zitatozwa na kuhesabiwa kama ada za Baraza pamoja na ada nyingine zinazolipwa katika Baraza.36. Kufunga utekelezaji wa hukumu
37. Utovu wa nidhamu wa dalali na msambaza nyaraka
Dalali na msambaza nyaraka ambaye atatenda kitendo cha utovu wa nidhamu—38. Masharti ya mpito TS Na.174 la mwaka 2003
Cheti kilichotolewa au idhini iliyotolewa kwa dalalichini ya Kanuni za Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya kitachukuliwa kuwa kimetolewa chini ya Kanuni hizi na kitaendelea kuwa halali hadi kitakapoisha muda wake au kufutwa kwa kadrii takavyokuwa.History of this document
26 January 2024 this version
17 March 2023
06 March 2023
Assented to