Kanuni za Hakimiliki na Hakishiriki (Kampuni za Ukusanyaji na Ugawaji wa Mirabaha), 2023
Government Notice 215 of 2023
There are outstanding amendments that have not yet been applied. See the History tab for more information.
Kanuni za Hakimiliki na Hakishiriki (Kampuni za Ukusanyaji na Ugawaji wa Mirabaha), 2023
Collections
Related documents
Tanzania
Copyright and Neighbouring Rights Act, 1999
Kanuni za Hakimiliki na Hakishiriki (Kampuni za Ukusanyaji na Ugawaji wa Mirabaha), 2023
Tangazo la Serikali 215 ya 2023
- Imechapishwa katika Gazette of the United Republic of Tanzania 10 hadi 24 Machi 2023
- Imeidhinishwa tarehe 6 Machi 2023
- Ilianza tarehe 24 Machi 2023
- [Hili ni toleo la hati hii kama ilivyokuwa kutoka 24 Machi 2023 hadi 14 Machi 2024.]
Sehemu ya kwanza – Masharti ya utangulizi
1. Jina
Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Hakimiliki na Hakishiriki (Kampuni za Ukusanyaji na Ugawaji wa Mirabaha), 2023.2. Tafsiri
Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo—“Sheria” maana yake ni Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki;“Bodi” maana yake ni bodi ya wakurugenzi ya Ofisi iliyoanzishwa hivyo chini ya Sheria;“haki za jumla” maana yake ni haki zote zinazotolewa kwenye Sheria;“madaraja ya kazi” maana yake ni kazi kama zilivyotajwa katika kifungu cha 5(2) cha Sheria;“kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha” ina maana iliyotajwa katika kifungu cha 4 cha Sheria;“Msimamizi wa Hakimiliki” maana yake ni mkuu wa Ofisi aliyeteuliwa kwa mujibu wa Sheria;“mkutano mkuu” maana yake ni mkutano mkuu wa mwaka au mkutano mkuu maalumu ambao wanachama wa kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha wanashiriki na kutumia haki zao za uanachama;“Ofisi” maana yake ni Ofisi ya Hakimiliki ya Tanzania iliyoanzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 46 cha Sheria;“ada ya usimamizi” maana yake ni kiasi kinachotozwa, kukatwa au kufidiwa na kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha kutokana na mapato yanayotokana na hakimiliki au kutokana na mapato yoyote ya uwekezaji wa mapato ya mauzo yanayozalishwa kutokana na hakimiliki ili kulipia gharama za usimamizi wa hakimiliki au haki zinazohusiana;“Waziri” ina maana Waziri kwa wakati huo mwenye dhamana na haki miliki na haki shiriki;“mwanachama” maana yake ni mmiliki wa hakimiliki au chombo kinachowawakilisha wenye hakimiliki, inajumuisha kampuni nyingine za kukusanya na kugawa mirabaha na chama cha wenye hakimiliki;“makubaliano ya uwakilishi” maana yake ni makubaliano baina ya kampuni za kukusanya na kugawa mirabaha ambapo kampuni moja inaipa kampuni nyingine madaraka ya kusimamia hakimiliki za wale inaowawakilisha;"mapato ya hakimiliki" maana yake ni mapato yanayokusanywa na kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha kwa niaba ya wenye hakimiliki, iwe yanatokana na hakimiliki pekee, haki ya malipo au haki ya fidia;"mrabaha" maana yake ni malipo ya kiwango kilichokubalika kwa mwenye hakimiliki kwa kutumia kazi yenye hakimiliki; na"mtumiaji" maana yake ni mtu anayenufaika na kazi kutokana na idhini ya wenye hakimiliki, malipo ya wenye hakimiliki au malipo ya fidia kwa wenye hakimiliki.[Sura ya 218]Sehemu ya pili – Utoaji wa leseni kwa kampuni ya kukusanya na kugawa miraba
3. Zuio la ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha
4. Maombi ya leseni
5. Uamuzi wa maombi
6. Utoaji wa leseni
7. Hatua zinazochukuliwa iwapo hakuna kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha katika baadhi ya madaraja
8. Kuondoa vigezo vya masharti ya leseni ya kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha
Endapo kuna mwombaji mmoja wa leseni ya kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha kwa daraja la kazi na maombi hayakidhi vigezo vyovyote vya utoaji wa leseni kwa mujibu wa Sheria na Kanuni hizi, Ofisi inaweza kuondoa vigezo hivyo kama itaona kwamba kuto tolewa kwa leseni kutaathiri utendaji kazi mzuri wa kampuni kuhusiana na daraja la kazi:Isipokuwa kwamba, Ofisi itaitaka kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha kutimiza vigezo vya maombi ya leseni ndani ya muda wa leseni utakaoelekezwa.9. Maombi ya kuhuisha leseni
10. Uamuzi wa maombi ya kuhuisha leseni
11. Utoaji wa leseni iliyohuishwa
Ofisi itampatia mwombaji aliyekubaliwa, leseni iliyohuishwa kwa kipindi cha mwaka mmoja kupitia Fomu CMO 4 iliyoainishwa katika Jedwali la Kanuni hizi.12. Kusimamisha au kubatilisha leseni
13. Rejesta na tangazo kwa umma
Sehemu ya tatu – Maadili ya kampuni za kukusanya na kugawa mirabaha
14. Maadili ya kampuni kwa ujumla
Sehemu ya nne – Uanachama na usimamizi wa kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha
15. Uanachama katika kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha
16. Kanuni za uanachama wa kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha
17. Uanachama na usimamizi wa kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha
Mwanachama, baada ya kutoa taarifa ya nia yake ya kujitoa, atakuwa na haki ya kujivua uanachama wake kwenye kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha au hakimiliki alizotoa kwa kampuni kuhusiana na kazi zake:Isipokuwa kwamba, Kampuni ya kukusanya na kugawa Mirabaha ambayo uanachama wake uko chini ya idadi ya wajumbe thelathini kutokana na wanachama kujitoa, itaitaarifu Ofisi ndani ya siku saba, na itasajili idadi ya wanachama inayohitajika ndani ya siku kumi na nne tangu siku ya taarifa kutolewa.18. Ushiriki wa wanachama
Kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha—19. Mikutano ya kampuni za kukusanya na kugawa mirabaha
20. Haki ya kupiga kura
Mwanachama katika mkutano mkuu atakuwa na haki ya kupiga kura kwa kufuata vigezo vifuatavyo:21. Ripoti za mikutano
Kila kampuni yenye leseni kwa mujibu wa Kanuni hizi ya kufanya kazi kama kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha itatoa ripoti yenye kumbukumbu na uamuzi uliofanywa katika kila mkutano wa mkutano mkuu na Bodi ili ziingizwe kwenye daftari maalumu lililowekwa kwa madhumuni hayo, na nakala ya ripoti iliyothibitishwa itawasilishwa katika Ofisi pale Ofisi itakapoihitaji.22. Hesabu, ripoti ya mwaka na ukaguzi
23. Muundo na maudhui ya ripoti ya mwaka
24. Akaunti ya akiba maalumu
25. Muda wa kuhifadhi fedha kwenye akaunti ya akiba maalumu
26. Wajibu wa kuripoti wa kampuni za kukusanya na kugawa mirabaha
27. Wajibu wa kutoa taarifa kwa watumiaji wa hakimiliki
28. Gharama za uendeshaji wa kampuni
29. Usimamizi wa kazi na mgongano wa maslahi
Sehemu ya tano – Utoaji leseni, ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha
30. Haki ya wenye leseni na upangaji wa ada
31. Kukusanya na kutumia mapato ya hakimiliki
32. Ugawaji fedha kwa wenye hakimiliki
33. Malipo ya mirabaha kwenye makubaliano ya uwakilishi
34. Makato
35. Ushughulikiaji wa hakimiliki zinazosimamiwa chini ya makubaliano ya uwakilishi
36. Wajibu wa mtumiaji
37. Taarifa zinazotolewa kwa kampuni nyingine za kukusanya na kugawa mirabaha
38. Utoaji wa taarifa kwa umma
Kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha itatangaza na kuhuisha taarifa zifuatazo katika tovuti yake:Sehemu ya nne – Utatuzi wa malalamiko na usuluhishi wa migogoro
[Tafadhali kumbuka: nambari imenakilliwa kama ilivyo katika hati asili.]39. Utatuzi wa malalamiko
40. Usuluhishi
41. Kamati ya uamuzi
42. Uamuzi wa kamati ya uamuzi
43. Rufaa dhidi ya uamuzi uliotokana na usuluhishi
Sehemu ya sita – Kuzingatia masharti
44. Uhitaji wa taarifa
45. Notisi ya kutozingatiwa kwa masharti
46. Adhabu kulipa fedha kutokana na ukiukwaji
47. Taratibu za utoaji wa adhabu ya fedha
48. Rufaa dhidi ya utozwaji wa adhabu ya fedha
49. Kutolipa adhabu wakati wa kusubiri rufaa
Endapo rufaa au hatua ya mahakama inatolewa dhidi ya uamuzi wa ofisi, upande unaowasilisha rufaa haulazimiki kulipa adhabu wakati wa kusubiri mashauri na uamuzi wa rufaa na adhabu hiyo ya kulipa haitatekelezwa wakati wa kusubiri rufaa.Sehemu ya saba – Masharti mengineyo
50. Fidia ya kutotumia leseni
Kila kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha itatoa fidia au utaratibu ambao utatumika ikitokea mtumiaji hawezi kutumia leseni aliyopewa na kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha, ambapo tukio hilo litakuwa limetokana na uzembe, uwasilishaji usio sahihi au kasoro nyingine zinazotokana na hilo au kusababishwa na kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha.51. Hatua dhidi ya maafisa wa kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha
52. Kanuni za kampuni
Kampuni inaweza kutengeneza kanuni za ustawi wa wanachama wake na kutenga si zaidi ya asilimia tano ya mirabaha yake yote iliyokusanywa kwa ajili ya utekelezaji wa kanuni kwa ufanisi, na kiasi hicho hakipaswi kugawanywa kwa watu wasiohusika kwa mujibu wa kanuni ya 30.53. Kufutwa kwa kanuni na masharti ya mpito
History of this document
15 March 2024 amendment not yet applied
24 March 2023 this version
06 March 2023
Assented to