Amri ya Kubadilisha Mamlaka ya Mahakama ya Wilaya Chato ya mwaka 2023

Government Notice 92 of 2023

Amri ya Kubadilisha Mamlaka ya Mahakama ya Wilaya Chato ya mwaka 2023

Tanzania
Magistrates’ Courts Act

Amri ya Kubadilisha Mamlaka ya Mahakama ya Wilaya Chato ya mwaka 2023

Tangazo la Serikali 92 ya 2023

[Imetolewa chini ya kifungu cha 4(3)]

1. Jina

Amri hii itajulikana kama Amri ya Kubadilisha Mamlaka ya Mahakama ya Wilaya Chato ya mwaka 2023.

2. Mabadiliko ya mamlaka ya Mahakama ya Wilaya ya Chato

Mamlaka ya Mahakama ya Wilaya Chato yanayotolewa chini ya Sheria ya Mahakama za Mahakimu yanabadilishwa kama ilivyoanishwa katika Jedwali la Amri hii kwa madhumuni ya kusikilizana kuamua mashauri ya ainazote yaliyondani ya mamlaka ya awali, rufaa na mapitio ya mahakama ya wilaya.[Sura ya 11]

3. Eneo la mamlaka

Mahakama ya Wilaya Chato, pamoja na mamlaka yake ndani ya Wilaya ya Chato, itakuwa na mamlaka katika eneo lililoainishwa katika Jedwali la Amri hii.

Jedwali (Limetengenezwa chini ya Aya ya 2 na 3)

Na.Mahakama ya wilayaEneo la mamlaka
1.Mahakama ya Wilaya ChatoWilaya ya Chato ikijumuisha Kisiwa cha Rubondo
▲ To the top

History of this document

17 February 2023 this version
08 February 2023
Assented to