Tanzania
Social Security (Regulatory Authority) Act, 2008
Kanuni za Matumizi ya Mafao ya Mwanachama kama Dhamana ya Mkopo wa Nyumba za Mwaka 2024
Tangazo la Serikali 149 ya 2024
- Imechapishwa katika Government Gazette 10 hadi 8 Machi 2024
- Imeidhinishwa tarehe 6 Februari 2024
- Ilianza tarehe 8 Machi 2024
- [Hili ni toleo la hati hii kutoka 8 Machi 2024.]
Sehemu ya kwanza – Masharti ya utangulizi
1. Jina
Kanuni hizi zitajulikana kama Kanuni za Matumizi ya Mafao ya Mwanachama kama Dhamana ya Mkopo wa Nyumba za Mwaka 2024.2. Tafsiri
Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo—“Bodi” maana yake ni Bodi ya Wadhamini ya Mfuko;“Divisheni” maana yake ni Divisheni inayohusika na masuala ya hifadhi ya jamii iliyopo ndani ya Wizara yenye dhamana na masuala ya hifadhi ya jamii;“Mfuko” ina maana iliyotolewa kwenye sheria ya mfuko husika;“michango” maana yake ni michango inayolipwa kwenye Mfuko kama ilivyoainishwa kwenye sheria za mifuko ya pensheni;“mwanachama” maana yake ni mwajiriwa au mfanyakazi aliyesajiliwa katika skimu na inajumuisha mwanachama anayestahili, au anayepokea, mafao chini ya skimu;“mwanachama anayestahili” maana yake ni mwanachama ambaye amechangia kwa kipindi kisichopungua miezi mia moja themanini ambapo kati ya miezi hiyo, michango ya miezi kumi na mbili ni lazima iwe imechangwa mfululizo kabla ya tarehe ya kutolewa kwa dhamana;“mwongozo wa uendeshaji” maana yake ni nyaraka ya ndani ya Mfuko inayoelekeza namna ya utekelezaji na utoaji wa dhamana za mikopo chini ya Kanuni hizi;“mkopo wa nyumba” maana yake ni mkopo unaotolewa kwa mwanachama anayestahili kwa malengo ya kununua, kujenga au kuboresha nyumba ya makazi ambayo imedhaminiwa na nyumba yenyewe kama dhamana ya kwanza;“Sheria” maana yake ni Sheria ya Hifadhi ya Jamii;[Sura ya 135]“taasisi” maana yake ni mabenki na taasisi nyingine za fedha zilizosajiliwa na kupata leseni chini ya Sheria ya Benki na Taasisi za Fedha.[Sura ya 342]Sehemu ya pili – Dhamana
3. Matumizi ya mafao kama dhamana
4. Kiwango cha mafao kwa ajili ya dhamana
Sehemu ya tatu – Masharti ya dhamana
5. Masharti ya dhamana kwa mwanachama
Mwanachama atakuwa na sifa ya kupata dhamana ya Mfuko kama amekidhi masharti yafuatayo:6. Masharti ya dhamana kwa taasisi
Taasisi itakayohitaji dhamana ya Mfuko kwa ajili ya mkopo kwa mwanachama itapaswa—7. Maombi ya idhini
8. Masharti ya utoaji wa mikopo
Sehemu ya nne – Kiwango cha dhamana
9. Kiwango cha dhamana
Kiwango cha dhamana ya mkopo wa nyumba chini ya Kanuni hizi hakitazidi asilimia hamsini ya mafao anayostahili mwanachama wakati wa kufanya maombi.10. Dhamana ya mkopo
Sehemu ya tano – Uhai wa dhamana
11. Uhai wa dhamana
Dhamana iliyotolewa chini ya Kanuni hizi itakuwa hai hadi yatakopotokea yafuatayo:12. Kutumika kwa dhamana
13. Usuluhishi wa migogoro
14. Taarifa
Mfuko utapaswa kuwasilisha taarifa kwenye Divisheni kwa kila robo mwaka ikionesha kiwango na idadi ya dhamana zilizotolewa, pamoja na maelezo ya malipo ya mikopo na dhamana zilizotumika na zilizoisha muda wake.Sehemu ya sita – Kuhama kwa mwanachama kutoka mfuko mmoja kwenda mwingine
15. Uhamisho kwenda kwenye mifuko
Uhamisho wa mwanachama kutoka Mfuko mmoja kwenda mwingine hautaathiri dhamana iliyotolewa chini ya Kanuni hizi.16. Ujumuishwaji
Mwanachama yeyote ambaye amechangia kwenye Mfuko zaidi ya mmoja, kwa madhumuni ya Kanuni hizi, atakuwa na haki ya kujumuisha vipindi vya uchangiaji wake kwa mujibu wa mwongozo wa ujumuishaji uliotolewa na Divisheni.History of this document
08 March 2024 this version
Commenced
06 February 2024
Assented to