Ask AI
Ask questions and understand this document faster using AI.
Tanzania
Railways Act, 2002
Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma binafsi, za Mwaka 2024
Tangazo la Serikali 214 ya 2024
- Imechapishwa katika Government Gazette kwa 29 Machi 2024
- Imeidhinishwa tarehe 20 Machi 2024
- Ilianza tarehe 29 Machi 2024
- [Hili ni toleo la hati hii kutoka 29 Machi 2024.]
Sehemu ya kwanza – Masharti ya utangulizi
1. Jina
Kanuni hizi zitajulikana kama Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma binafsi, za Mwaka 2024.2. Matumizi
Kanuni hizi zitatumika kwa ajili ya kuweka utaratibu wa matumizi ya miundombinu ya reli kwa watoa huduma binafsi.3. Tafsiri
Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo—"mkataba wa matumizi" maana yake ni mkataba wa matumizi kati ya Msimamizi wa Miundombinu na mtoa huduma na inajumuisha viambatisho na vielelezo husika;“haki ya matumizi ya miundombinu” maana yake ni haki ya kutumia miundombinu ya reli ikiwemo mapito ya reli, kama ilivyoombwa na mtoa huduma;"ada ya matumizi ya miundombinu" maana yake ni ada inayoamuliwa kwa mujibu wa mkataba wa matumizi inayolipwa na mtoa huduma kwa Msimamizi wa Miundombinu kwa ajili ya haki ya matumizi ya miundombinu, na inajumuisha faida na tozo yoyote inayolipwa kuhusiana na ada hiyo;"Sheria" maana yake ni Sheria ya Reli;[Sura ya 170]"maombi maalumu" maana yake ni maombi ya kutumia njia ya treni kwa wakati maalumu tofauti na ratiba ya kawaida ya mchakato wa ugawaji wa njia ya reli;“mpango wa utozaji” maana yake ni taratibu mahususi za utozaji zilizowekwa kwa mujibu wa Kanuni hizi, Mdhibiti wa Reli au Msimamizi wa Miundombinu kadiri itakavyokuwa;“mfumo wa utozaji” maana yake ni mfumo ulioanzishwa na Msimamizi wa Miundombinu ili kubainisha ada ya matumizi ya miundombinu;“Msimamizi wa Miundombinu” maana yake ni Shirika lililoanzishwa kwa mujibu wa Sheria;[Sura ya 170]“leseni” maana yake ni leseni ya matumizi ya reli inayotolewa na Mdhibiti;“Waziri” itakuwa na maana sawa na iliyoainishwa katika Sheria;[Sura ya 170]“Maelezo ya mtandao wa reli” maana yake ni maelezo kuhusu masharti ya jumla, miongozo, taratibu na vigezo vya upangaji wa ada kwaajili ya matumizi ya miundombinu ya reli kwa watoa huduma binafsi;“matumizi ya miundombinu ya reli kwa watoa huduma binafsi” itakuwa na maana sawa na iliyoainishwa katika Sheria"mtoa huduma" maana yake ni mtu ambaye amepewa leseni kutoa huduma za reli kupitia taratibu za matumizi ya miundombinu ya reli kwa watoa huduma binafsi;“kibali” maana yake ni kibali cha matumizi ya reli kinachotolewa na Msimamizi wa Miundombinu; na"Mdhibiti" itakuwa na maana sawa na iliyoainishwa katika Sheria.[Sura ya 170]Sehemu ya pili – Maombi ya kibali na leseni
4. Maombi ya kibali
5. Ada za kibali
Mwombaji wa kibali atalipa kwa Msimamizi wa Miundombinu ada ya maombi kama ilivyoainishwa katika Jedwali la Pili ambapo, ada hizo zinaweza kubadilishwa na Mdhibiti mara kwa mara kwa mujibu wa masharti ya Sheria hii.6. Maombi ya leseni
7. Ada za leseni
Baada ya Maombi ya leseni kukubaliwa, mtoa huduma atapaswa kulipa ada za leseni kama zilivyoainishwa katika Jedwali la Pili la Kanuni hizi.8. Muda wa leseni
Sehemu ya tatu – Upatikanaji wa miundombinu na huduma za reli
9. Haki ya matumizi ya miundombinu
Mtoa huduma ana haki sawa ya kutumia miundombinu kwa ajili ya uendeshaji wa aina yoyote ya shughuli za reli.10. Matumizi ya vituo na bandari
11. Upatikanaji wa huduma
Sehemu ya nne – Usimamizi na uendeshaji wa miundombinu
12. Uhuru wa usimamizi
Mtoa huduma atadumisha hadhi ya mwendeshaji huru katika usimamizi wa shughuli zake za kutoa huduma ya reli.13. Mpango wa biashara
14. Maelezo ya mtandao wa miundombinu
Sehemu ya tano – Tozo za miundombinu
15. Kuanzisha, kupanga na kukusanya tozo
16. Mpango wa utendaji kazi
17. Tozo kwa miundombinu isiyotumika
Msimamizi wa Miundombinu anaweza kutoza tozo atakazoona zinafaa kwa uwezo ulioombwa na kutotumika, na atatoa motisha kwa matumizi bora ya uwezo.Sehemu ya sita – Mgawanyo wa matumizi ya miundombinu ya reli
18. Maombi ya mgao wa miundombinu
19. Ratiba ya uendeshaji
20. Kutohamishika
21. Mgao usio na upendeleo
Msimamizi wa Miundombinu atahakikisha kwamba mgao wa matumizi ya miundombinu unatolewa kwa misingi ya haki na isiyo ya upendeleo, na mkataba unaoingiwa ni wa uwazi na kwa kuzingatia matakwa ya Kanuni hizi.22. Kupanga na kuratibu
23. Mkataba wa matumizi ya miundombinu
24. Maombi ya dharura
25. Tamko la miundombinu maalumu
Msimamizi wa Miundombinu anaweza kutenga sehemu fulani za miundombinu kwa ajili ya matumizi ya aina maalumu za huduma ya reli na, mara tu miundombinu itakapotengwa, anaweza kutoa kipaumbele kwa aina hiyo maalumu ya huduma ya reli katika mgao wa miundombinu.26. Msongamano katika miundombinu
27. Uchambuzi wa uwezo wa miundombinu
28. Mpango wa kuimarisha uwezo wa miundombinu
29. Matumizi ya njia za treni
30. Hatua maalum za kuchukua wakati wa dharura
Sehemu ya saba – Udhibiti na rufaa
31. Mamlaka ya udhibiti
32. Uwasilishaji wa malalamiko kwa Mdhibiti
33. Masuala ya ushindani
Mdhibiti atawajibika kukuza ushindani wa haki katika huduma za reli na kuzuia vitendo vinavyokiuka misingi ya ushindani katika soko la huduma za reli.34. Uwezo wa kupata taarifa
Mdhibiti atakuwa na uwezo wa kupata taarifa zinazohusiana na majukumu na kazi zake kutoka kwa Msimamizi wa Miundombinu, watoa huduma na wadau wengine.Sehemu ya nane – Masharti ya jumla
35. Masharti ya leseni
Kwa kuzingatia Kanuni hizi, mtoa huduma atahakikisha—36. Uchunguzi na uchambuzi wa ajali
37. Uwajibikaji
Baada ya kukamilika kwa uchunguzi, aliyesababisha ajali atawajibika kulipa fidia ndani ya siku sitini kuanzia tarehe ya kukamilika kwa uchunguzi.38. Shughuli za uokoaji
Katika tukio la ajali inayohusisha treni ya mtoa huduma, kazi za uokoaji ili kurejesha shughuli za uendeshaji zitafanywa na Msimamizi wa Miundombinu kwa mujibu wa mipango ya dharura na itakuwa katika gharama za ziada.39. Kusitishwa na kufutwa kwa kibali
40. Kusitishwa na kufutwa kwa leseni
41. Matumizi na uhifadhi wa kibali au leseni
42. Taarifa ya ukiukwaji
43. Ukaguzi wa kibali au leseni
Mdhibiti au mtu mwingine yeyote aliyeidhinishwa na Mdhibiti anaweza kuamuru mtu mwenye leseni, kibali au idhini chini ya Kanuni hizi kuwasilisha kwa ajili ya ukaguzi.Sehemu ya tisa – Makosa na adhabu
44. Makosa na adhabu
History of this document
29 March 2024 this version
Commenced
20 March 2024
Assented to