This is the latest version of this Government Notice.
Ask AI
Ask questions and understand this document faster using AI.
Tanzania
Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2024
Kanuni za Mashauri ya Uchaguzi wa Wabunge za Mwaka, 2025
Tangazo la Serikali 431 ya 2025
- Imechapishwa katika Subsidiary Legislation Supplement kwa 11 Julai 2025
- Imeidhinishwa tarehe 10 Julai 2025
- Ilianza tarehe 11 Julai 2025
- [Hili ni toleo la hati hii katika 25 Oktoba 2025.]
- [Note: This legislation was revised and consolidated as at 31 July 2002 and 30 November 2019 by the Attorney General's Office, in compliance with the Laws Revision Act No. 7 of 1994, the Revised Laws and Annual Revision Act (Chapter 356 (R.L.)), and the Interpretation of Laws and General Clauses Act No. 30 of 1972. All subsequent amendments have been researched and applied by Laws.Africa for TANZLII.]
- [Iliyorekebishwa na Kanuni za Marekebisho ya Kanuni za Mashauri ya Uchaguzi wa Wabunge za Mwaka 2025 (Tangazo la Serikali 610 ya 2025) hadi 17 Oktoba 2025]
Sehemu ya kwanza – Masharti ya utangulizi
1. Jina
Kanuni hizi zitajulikana kama Kanuni za Mashauri ya Uchaguzi wa Wabunge za Mwaka 2025.2. Tafsiri
Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo—“mahakama” maana yake ni Mahakama Kuu ya Tanzania au Mahakama Kuu ya Zanzibar, kadri inavyowezakuwa;“mtendaji wa uchaguzi” maana yake ni kama ilivyotafsiriwa na Sheria;“msajili” maana yake ni msajili au mrajisi wa mahakama, kaimu msajili au kaimu mrajisi, naibu msajili au kaimu naibu msajili; na“Sheria” maana yake ni Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani.[Sura ya 343]Sehemu ya pili – Uwasilishaji wa shauri la uchaguzina dhamana ya gharama za shauri
3. Kupinga uchaguzi
Uchaguzi wa Mbunge utapingwa kwa njia ya shauri la uchaguzi.4. Anayeweza kufungua shauri la uchaguzi
Shauri la uchaguzi linaweza kuwasilishwa na mtu yeyote aliyebainishwa chini ya kifungu cha 140(1) cha Sheria.5. Muundo na maudhui ya hati ya shauri
6. Wahusika katika shauri
7. Kuongeza au kubadilisha wahusika katika shauri
Endapo Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni mhusika pekee katika shauri na kwa madhumuni ya kuamua masuala husika mahakama inaona inafaa au ni muhimu mgombea aliyeshindwa au mtu mwingine yeyote aunganishwe kuwa mhusika katika shauri, mahakama inaweza kutoa amri ya kumuunganisha mgombea aliyeshindwa au mtu huyo mwingine kuwa mhusika katika shauri, na amri hiyo itakapotolewa, shauri litaahirishwa hadi wakati ambapo mtu ambaye anapaswa kuunganishwa katika shauri amepewa nakala ya hati ya shauri.8. Kuwasilisha hati ya shauri
9. Kukataliwa au kurekebishwa kwa hati ya shauri wakati wa uwasilishaji
10. Kupeleka hati ya shauri na kuwasilisha majibu
11. Dhamana ya gharama za shauri
Sehemu ya tatu – Orodha ya kura zinazopingwa na malalamiko dhidi ya matokeo ya uchaguzi katika kituo cha uchaguzi
12. Orodha ya kura zinazopingwa
13. Malalamiko dhidi ya matokeo ya uchaguzi katika kituo cha uchaguzi
14. Kupanga tarehe ya kusikiliza shauri
Sehemu ya nne – Utaratibu wa kusikiliza mashauri ya uchaguzi
15. Mahali na muda wa usikilizwaji wa shauri
16. Kuunganisha mashauri
Endapo mashauri mawili au zaidi yamewasilishwa kuhusiana na uchaguzi mmoja, mahakama inaweza kuelekeza kwamba baadhi au mashauri hayo yote yaunganishwe na kusikilizwa kama shauri moja.17. Shauri kusikilizwa na Jaji zaidi ya mmoja
18. Utoaji wa nyaraka
Wahusika katika shauri au mawakili wao watawasilisha, kabla au wakati wa usikilizaji wa awali, nyaraka zote wanazokusudia kuzitoa kama ushahidi wakati wa usikilizaji wa shauri ambazo hazikuambatishwa kwenye hati ya shauri au kwa namna yoyote ile hazijawasilishwa mahakamani, na nyaraka ambazo mahakama imeamuru ziwasilishwe.[TS Na. 610 la 2025 k. 4]19. Usikilizwaji wa awali
20. Uainishaji wa hoja bishaniwa
Baada ya usikilizaji wa awali kukamilika, mahakama itaainisha masuala ambayo wahusika wa shauri wanabishania na kuandika hoja bishaniwa ambazo uamuzi sahihi wa shauri unaonekana kuzitegemea.21. Usikilizwaji wa Shauri
22. Utaratibu wa kusikiliza shauri
23. Shahidi wa mahakama
24. Matumizi ya Sheria ya mwenendo wa mashauri ya madai Sura ya 33 na Sura ya 8 ya Zanzibar
Kwa kuzingatia masharti ya Sheria na Kanuni hizi, usikilizaji, utaratibu na mwenendo wa shauri utatumia, kwa kuzingatia maboresho muhimu kwa kadri yatakavyohitajika, kanuni zinazosimamia utaratibu na mwenendo wa mashauri ya madai kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Madai na Amri ya Mwenendo wa Mashauri ya Madai.25. Sababu ambazo hazikuainishwa kwenye hati ya shauri
Mlalamikaji hataleta hoja au kusikilizwa kuhusiana na sababu yoyote ambayo haikuainishwa katika hati ya shauri, isipokuwa kwa ruhusa ya mahakama.26. Kuahirishwa kwa usikilizwaji wa shauri
27. Katazo la kuahirisha shauri
Usikilizwaji wa shauri unapoanza, utaendelea mfululizo, isipokuwa kama mahakama itaona kuwa kuahirishwa kwa usikilizwaji zaidi ya siku inayofuata ni muhimu kwa sababu zitakazoandikwa katika mwenendo wa shauri.28. Jaji kushindwa kuendelea na shauri
29. Mlalamikaji kushindwa kuhudhuria
30. Mlalamikiwa kushindwa kuhudhuria
31. Kuhudhuria kupitia wakili
Kwa madhumuni ya Kanuni hizi, kuhudhuria kwa wakili kutachukuliwa kuwa ni kuhudhuria kwa mhusika wa shauri anayewakilishwa.32. Kuondoa shauri
33. Ukomo wa shauri
34. Shauri kutotupiliwa mbali kwa sababu ya kasoro ya kiutaratibu
35. Ada
36. Kufutwa kwa Kanuni
Kanuni za Mashauri ya Uchaguzi wa Kitaifa za Mwaka 2020 zinafutwa.[TS. Na. 782 la 2020, 934 la 2020, 610 la 2025 k. 8]History of this document
25 October 2025 this version
Consolidation
17 October 2025
11 July 2025
10 July 2025
Assented to




